Alhamisi, 7 Januari 2016

JIFUNZE HAPA

 ***SIMULIZI YENYE MAZINGATIO***
...Aboubakar ni mwajiriwa katika
kampuni moja ya usambazaji wa
nyama.
Siku moja jioni baada ya

kumaliza kazi zake za siku
aliamua aingie katika chumba
baridi cha kuhifadhia nyama
kukagua kitu na kwa bahati
mbaya mlango ukajifunga huku
akiwa ndani.
Alijaribu kugonga mlango na
hata kupiga kelele za kuomba
msaada kwa muda mrefu lakini
jitihada zake hazikufanya lolote
kwani kutokana na barafu
zilizomo ndani na jinsi........................
.ENDELEA MBELE
kulivyozibwa kuzuia ubaridi
kutotoka nje haikuwa rahisi kilio
chake cha kuomba msaada
kusikika.
Haikuwa rahisi kusikika sauti yake
kutoka katika chumba hicho na
kila mfanyakazi alikuwa
ameshaondoka.
Masaa manne baadae
Aboubakar alikuwa kama yuko
katika bonde la umauti akisubiri
kifo chake huku akimwomba
Mungu wake kwa sala yenye
unyenyekevu mkubwa.
Akiwa katikati ya sala yake mara
akashtushwa kuona mlango wa
chumba hicho ukifunguliwa na
mlinzi wa kampuni hiyo akiingia
na kumwokoa.
Wakiwa katika chumba kingine
huku Aboubakar akiwa kapewa
msaada wa moto ili kuupasha
mwili wake joto na kahawa ikiwa
Mezani, Aboubakar akaamua
amuulize yule mlinzi ni kitu gani
kilimfanya akifungue chumba
kile.
Mlinzi akamjibu, " nimefanya kazi
katika kampuni hii kwa miaka 21
na katika kipindi hiki mamia ya
wafanyakazi wamekuwa
wakiniona kama mtu nisiye na
maana na ni wachache sana
wanaonisalimia kwa kuniambia
HABARI ZA ASUBUHI wakiwa
wanaingia kazini na KAZI NJEMA
wanapoondoka jioni kurudi
makwao.
Leo asuhuhi ulipoingia
ulinisalimia kwa furaha kama
kawaida yako na jioni wakati
watu wanaondoka kurudi kwao
nikaisubiri sauti yako kunifariji
tena kwa kusema KAZI NJEMA
kama siku nyingine lakini
sikuisikia ndio nikaamua kuanza
kupitia kila chumba kuona nini
kimekupata na ndio nikakuona
kwenye chumba kile ukiwa
umefungiwa"
Aboubakar kwa furaha yenye
maumivu alibubujikwa na
machozi katika macho yake.
Funzo
Mthamini aliyejuu na aliye chini
yako, kwani yajayo huyajui, bali
unayajua yalopita tuu.
Tuishi maisha ya kupendana na
kuwajali wale watuzungukao
kwani huwezi jua ni namna gani
kwa kufanya hivyo tunawapa
furaha katika maisha yao na
kuwafariji.
UPENDO NI NGUZO MUHIMU
KTK MAISHA

By.. kisleu.com